Play Icon - Donate X Webflow Template
Watch video

Kituo cha Mafunzo kwa Mkulima (FTC) - Vianzi

Kituo cha Mafunzo kwa Mkulima (FTC), pamoja na kutoa mafunzo ni shamba la kilimo hai ambapo mbinu zote jumuishi za kilimo cha mazao ya msimu, uzalishaji wa nafaka kwa kutegemea mvua, ufugaji wa mifugo, kilimo misitu zinatekelezwa. Kituo hiki kipo eneo la Vianzi, kijiji kilicho umbali wa km 25 kutoka Morogoro mjini. FTC ni mahali pekee pakujifunza mbinu za kilimo hai. Aina mbalimbali za mafunzo hutolewa kwa wakulima binafsi, wakulima na wataalamu kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs), mashirika ya kijamii (CBOs) na sekta ya umma.

Tulianzaje?

Kituo cha Mafunzo ya Mkulima (FTC) cha SAT kilifunguliwa rasmi Septemba 14, 2013, na kimeendesha kozi mbalimbali za mafunzo zilizohudhuriwa na wakulima na wataalamu kutoka Tanzania, Malawi, Kenya, na nchi za Ulaya. Tathmini na maoni kutoka kwa washiriki yamekuwa ya kutia moyo tangu hapo na yamekuwa daima kichocheo kwetu kuimarisha ubora wa kozi zetu.

KOZI ZINAZOTOLEWA KITUONI 

Kozi zetu

Uzalishaji wa Uyoga

9th June - 13th June 2025

4th August - 8th August 2025 (OTP)

Kadri mienendo ya chakula duniani inavyobadilika na mahitaji ya chakula bora na lishe yanavyoongezeka, kilimo cha uyoga kinatokea kama biashara endelevu na yenye faida. Kozi hii imeundwa kukuletea ulimwengu wa kilimo cha uyoga cha kikaboni, eneo ambalo si tu linaleta mapato mengi lakini pia linatumia rasilimali za kilimo kwa ufanisi.

Kozi ya usindikaji na Kuongeza thamani ya maziwa

2nd June - 6th June 2025

Jisajili sasa kwenye Kozi ya Kozi ya usindikaji na Kuongeza thamani ya maziwa

Usimamizi Endelevu wa Taka na mboji

7 Julai -  11 Julai 2025

20 Oktoba - 24 Oktoba 2025

Jisajili sasa kwenye Kozi ya Usimamizi Endelevu wa Taka na Komposti na ugundue jinsi ya kutumia taka kama rasilimali yenye thamani.

MAFUNZO KWA WAKUFUNZI WAWEZESHAJI

21 Julai - 25 Julai 2025

13 Oktoba - 18 Oktoba 2025

Je! unataka kuwa mwezeshaji imara katika kilimo?

Uhifadhi na usimamizi wa mazao baada ya kuvuna

1 Disemba – 5 Disemba 2025

Jifunze jinsi ya Kuhifadhi Mazao Baada ya Kuvuna na umuhimu wa kuhifadhi mazao yako

UCHAKATAJI WA VYAKULA NA UONGEZAJI THAMANI

27 Oktoba - 31 Oktoba 2025

Bidhaa zilizochakatwa na kuongezwa thamani huwa na bei nzuri, pia zinaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu, na zinachukua nafasi ndogo kwenye kuhifadhiwa.

KILIMO HIFADHI

1 Septemba - 5 Septemba 2025

Endeleza shughuli zako za kilimo huku ukilinda mazingira ndio kusudi la mafunzo haya.

KILIMO CHA KUDUMU

18 Agosti – 29 Agosti 2025

Kilimo cha kudumu ni kozi inayotambulika kimataifa, inayoendeshwa kwa muda wa wiki mbili na utafanikiwa kupata Cheti cha kilimo cha Kudumu. Mafunzo haya yanatoa utangulizi wa kilimo cha kudumu ilivyofafanuliwa na mwanzilishi wake Bwana Bill Mollison.

UJASIRIAMALI NA KILIMO BIASHARA

1 Septemba – 5 Septemba 2025

Je, una nia ya kuanzisha biashara ya kilimo yenye mafanikio?

MADAWA YA ASILI KWA TIBA ZA BINADAMU

10 Novemba – 14 Novemba 2025

Je! Unajua nguvu ya mimea?

KILIMO HAI HATUA YA PILI

13 Oktoba – 17 Oktoba 2025

Mafunzo ya kati ya kilimo endelevu

Kilimo hai hatua ya tatu

20 Oktoba - 24 Oktoba 2025

24 Novemba - 28 Novemba 2025

Kilimo ikolojia hutumia rasilimali za asili ili kwa uzalishaji wa chakula bora na mifugo.

KAMBI YA VIJANA YA KILIMO

11 Agosti – 15th Agosti 2025

8 Septemba - 12 Septemba 2025

Je, kilimo ni biashara yenye faida kubwa ambayo vijana wanaweza kuwekeza?

UZALISHAJI WA MAZAO YA VIUNGO KWA MFUMO WA KILIMO HAI

22 Septemba -26 Septemba 2025, 3 Novemba – 7 Novemba 2025, 24 Novemba - 28 Novemba 2025

Mahitaji ya mazao ya viungo ya kilimo hai yanazidi kuongezeka duniani kote na yanatarajiwa kuongezeka maradufu ndani ya miaka mitano ijayo.

Misingi ya kilimo hai

6 Oktoba - 10 Oktoba 2025

17 Novemba - 21 Novemba 2025

Elewa misingi ya kilimo hai

MSINGI YA UZALISHAJI WANYAMA

14 Julai– 18 Julai 2025

15 Septemba - 20 Septemba 2025

Je unafahamu, ufugaji na uzalishaji wa mazao unaweza kufanyika kwa Pamoja?