Kilimo Hai!
Mifugo Bora!

Kilimo hai ni mfumo wa kilimo ambao hutumia mbinu za kuhifadhi na kukuza rutuba ya udongo, kuhifadhi viumbehai na kudhibiti visumbufu (wadudu, magonjwa na magugu) bila kutumia kemikali zinazo athiri mazingira yetu.

Mafanikio ya Shirika la SAT

500,000+
miti tuliyopanda
3000+ ekari
za shamba ambalo linatunzwa na kutumiwa kwa kuzingatia misingi ya kilimo hai
50,000+
wakulima waliofikiwa moja kwa moja na shirika katika maeneo yao
8000+
wahitimu waliopata mafunzo mbalimbali katika kituo chetu cha mafunzo kwa mkulima (FTC)-Vianzi
90,000
majarida ya MkM tunayochapisha na kuyasambaza kila baada ya miezi miwili
2000+
wakulima wa kilimo hai

Shirika la Kilimo Endelevu Tanzania (SAT)

Ni shirika lisilo la kiserikali na dira yake ni kuwa na wakulima wengi wanaoutumia mbinu za kilimo endelevu ili kuboresha maisha yao, na kuhifadhi mazingira.

Dhamira Yetu

  • Kuboresha mbinu za kilimo nchini Tanzania kwa kusambaza elimu sahihi ya kilimo endelevu
  • kuwajengea uwezo wakulima ili washiriki kikamilifu katika mnyororo wa thamani
  • kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta za umma na binafsi 
  • kuwa shirika linalotambulika kwa kufanya shughuli zake kwa uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika kuleta mageuzi ya kilimo, yaliyo rafiki kwa mazingira na yenye manufaa kiuchumi.

Huduma zinazotolewa na shirika la SAT

Kituo cha Mafunzo kwa Mkulima (FTC)- Vianzi

Shirika la SAT lilianzisha kituo cha kwanza cha mafunzo ya kilimo hai kwa mkulima, wajasiriamali, maafisa ugani na wafanyanyakazi nchini Tanzania kilichopo Kijiji cha Vianzi mkoani Morogoro mnamo mwaka 2013. Kituo hiki hutoa mafunzo mbalimbali zaidi ya kumi na nne (14+) kwa kutilia mkazo mafunzo kwa vitendo. Kituo kina eneo lenye ukubwa wa ekari 918,na hutoa huduma za malazi,chakula na usafiri kwa washiriki wote wa mafunzo. Mpaka sasa wakulima Zaidi ya 8000 wamepatiwa  mafunzo katika kituo hiki.

Jarida la Mkulima Mbunifu (MkM)

Kwa kupitia jarida la MkM, SAT huwafikia wakulima wadogo na wadau wengine wa kilimo wasiopungua 180,000 kila mwezi. MkM huchapisha mada zinazoelekeza mafunzo kwa vitendo, yanayoeleweka kwa urahisi. Jarida hili limekuwa likichapishwa kwa  zaidi ya miaka kumi, na ni jarida la muda mrefu zaidi na huchapisha mada mahususi za kilimo hai nchini Tanzania.

Linaaminiwa na wasomaji wake na kusaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi ili kuzalisha chakula bora kwa ajili ya familia zao, jamii na masoko. Shirika la SAT ndio wachapishaji wa jarida hili na hutumika kama njia ya kuwapasha habari wakulima wake.

Upunguzaji hewa ukaa kwa manufaa yetu (Fair Carbon 4 Us)

Changia kudhibiti ongezeko la hewa ukaa (CO2) kwa kupanda miti kupitia wakulima wetu. Kwa mchango wako, wakulima wadogo watawezeshwa kupanda miti kupitia kipato kidogo utakachochangia ili kutunza mazingira.  Je utapanda miti mingapi?

Biashara ya kijamii - SAT Holistic Group LTD

Shirika la kilimo Endelevu Tanzania (SAT) ni mwangalizi na mshauri wa kampuni ya SAT Holistic Group Ltd ambayo ni kampuni ya kijamii inayomilikiwa na ushirika wa wakulima. Kampuni hii huwaunganisha  wakulima zaidi ya 3,500 na masoko ya ndani na nje ya nchi, na huhamasisha matumizi ya mbinu endelevu za kilimo ili kupunguza umaskini.

SAT Holistic Group Ltd inamilikiwa na wakulima kwa asilimia 45%, wawekezaji wa kimkakati kwa 25% na waanzilishi (30%). Wajumbe wa bodi ni wakulima wenyewe.